Biblia Habari Njema

Luka 19:38-41 Biblia Habari Njema (BHN)

38. wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”

39. Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”

40. Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”

41. Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia