Biblia Habari Njema

Luka 19:30-34 Biblia Habari Njema (BHN)

30. akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwanapunda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungueni, mkamlete hapa.

31. Kama mtu akiwauliza kwa nini mnamfungua, mwambieni, ‘Bwana anamhitaji.’”

32. Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.

33. Walipokuwa wanamfungua yule mwanapunda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwanapunda huyu?”

34. Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”