Biblia Habari Njema

Luka 18:24-29 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, “Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika ufalme wa Mungu!

25. Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”

26. Wale watu waliposikia hayo, wakasema, “Nani basi, atakayeokolewa?”

27. Yesu akajibu, “Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu.”

28. Naye Petro akamwuliza, “Na sisi, je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!”

29. Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au ndugu au wazazi au watoto kwa ajili ya ufalme wa Mungu,