Biblia Habari Njema

Luka 17:14-20 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajioneshe kwa makuhani.” Basi, ikawa walipokuwa wanakwenda, wakatakasika.

15. Mmoja wao alipoona kwamba ameponywa, alirudi akimtukuza Mungu kwa sauti kubwa.

16. Akajitupa chini mbele ya miguu ya Yesu huku akimshukuru. Huyo alikuwa Msamaria.

17. Hapo Yesu akasema, “Je, si watu kumi walitakaswa? Wale tisa wako wapi?

18. Hakupatikana mwingine aliyerudi kumtukuza Mungu ila tu huyu mgeni?”

19. Halafu akamwambia huyo mtu, “Simama, uende zako; imani yako imekuponya.”

20. Wakati mmoja, Mafarisayo walimwuliza Yesu, “Ufalme wa Mungu utakuja lini?” Naye akawajibu, “Ufalme wa Mungu hauji kwa namna itakayoweza kuonekana.