Biblia Habari Njema

Luka 12:12-15 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”

13. Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”

14. Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi kuwa mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”

15. Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uhai wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”