Biblia Habari Njema

Luka 1:36-40 Biblia Habari Njema (BHN)

36. Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.

37. Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”

38. Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.

39. Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yudea.

40. Huko, aliingia katika nyumba ya Zakaria, akamsalimu Elisabeti.