Biblia Habari Njema

2 Wakorintho 4:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Basi, Mungu, kwa huruma yake, ametukabidhi kazi hii na hivyo hatufi moyo.

2. Tumeyaacha kabisa mambo yote ya aibu na ya kisirisiri. Hatuishi tena kwa udanganyifu, wala kwa kulipotosha neno la Mungu; bali kwa kuudhihirisha ukweli twajiweka chini ya uamuzi wa dhamiri za watu mbele ya Mungu.

3. Maana, kama Habari Njema tunayohubiri imefichika, imefichika tu kwa wale wanaopotea.

4. Hao hawaamini kwa sababu yule mungu wa ulimwengu huu amezitia giza akili zao wasipate kuuona wazi mwanga wa Habari Njema ya utukufu wa Kristo, ambaye ni mfano kamili wa Mungu.

5. Maana hatujitangazi sisi wenyewe, ila tunamhubiri Yesu Kristo aliye Bwana, sisi wenyewe tukiwa watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.