Biblia Habari Njema

2 Wafalme 13:19-21 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Elisha alikasirika sana, akamwambia mfalme, “Mbona hukupiga mara tano au sita? Hivyo ungewaangamiza Waaramu kabisa. Lakini sasa utawashinda mara tatu tu.”

20. Elisha alifariki, akazikwa.Kila mwaka, makundi ya Wamoabu yalikuja kuishambulia nchi ya watu wa Israeli.

21. Wakati mmoja, wakati wa mazishi, watu waliona kundi mojawapo la watu waliobeba maiti wakamtupa yule maiti kaburini mwa Elisha na kukimbia. Mara maiti huyo alipogusa mifupa ya Elisha, alifufuka na kusimama wima.