Biblia Habari Njema

2 Wafalme 10:34-36 Biblia Habari Njema (BHN)

34. Matendo mengine yote ya Yehu na vitendo vyake vya ushujaa yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Nyakati za Wafalme wa Israeli.

35. Akafariki na kuzikwa Samaria. Mwanae Yehoahazi akatawala mahali pake.

36. Yehu alitawala Israeli akiwa Samaria kwa miaka ishirini na minane.