Biblia Habari Njema

1 Wafalme 4:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Solomoni alikuwa mfalme wa nchi yote ya Israeli,

2. na wafuatao walikuwa baadhi ya maofisa wake wa vyeo vya juu: Azaria, mwana wa Sadoki, alikuwa kuhani.

3. Elihorefu na Ahiya wana wa Shausha, walikuwa makatibu; Yehoshafati mwana wa Ahiludi, alikuwa mweka kumbukumbu za habari.

4. Benaya mwana wa Yehoyada, alikuwa jemadari wa jeshi; nao Sadoki na Abiathari, walikuwa makuhani.