12. Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na fedha.Faida ya maarifa ni kwamba hekima hulinda maisha ya mtu aliye nayo.
13. Tafakarini vema kazi yake Mungu;ni nani awezaye kunyosha alichopinda Mungu?
14. Katika siku za fanaka uwe na furaha; katika siku za maafa utafakari jambo hili: Fanaka, pia maafa, Mungu amefanya hiyo ya kwanza iambatane na ya pili ili binadamu asiweze kujua yatakayotukia baada yake.